Thursday, March 5, 2015

Thursday, March 05, 2015
DSCN9215
Mkurugenzi Mtendaji wa Kliniki ya kimataifa ya afya ya uzazi kwa baba, mama, mtoto na vijana (AMM), Dk Ali Mzige (katikati) akizungumza na wandishi wa habari (hawapo pichani) juu ya Kambi ya kupima afya bila malipo kwa watoto wadogo, itakayofanyika Jumapili ya Machi 8 mwaka huu. Kushoto kwake ni Mwenyekiti wa umoja wa jamii ya watu kutoka India Bengali waliopo hapa Tanzania, BANGO SANGHO, Amit Nandy na kulia ni mwakilishi wa shule ya Kibugumu, Mwalimu Mzamili Ally.


Hayo yamesemwa jana Machi 4, jijini Dar es Salaam, na Mkurugenzi Mtendaji wa Kliniki ya kimataifa ya afya ya uzazi kwa baba, mama, mtoto na vijana (AMM), Dk Ali Mzige mbele ya wandishi wa habari wakati wa kutoa taarifa juu ya kambi ya upimaji wa afya kwa watoto wa chini ya umri wa miaka 5, itakayofanyika Jumapili ya Machi 8, katika shule ya Msingi Kibugumu iliyopo Kigamboni, wilaya ya Temeke.
Dk. Mzige alibainisha kuwa kama ilivyo kwa watu wazima, upimaji wa afya ya watoto wenye umri chini ya miaka 5 una manufaa makubwa kwa mtoto, familia na jamii ya watanzania wote.
Ambapo alibainisha kuwa, tatizo la utapia mlo kwa watoto hapa nchini imepelekea Tanzania kuwa nafasi ya tatu katika Bara la Afrika, Lishe duni kwa watoto na wajawazito huku Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) ikiongoza na Ethiopia ikiwa ni ya pili kwa tatizo hilo la utapiamlo.
Pia alieleza kuwa tatizo lingine ni la utapiamlo la kula chakula kupita kiasi kama vyakula vyenye wanga na sukari kwa wingi, mafuta kwa wingi na kuleta maradhi/magonjwa yasiyo ya kuambukiza kwa watoto na watu wazima.
Aidha, Dk. Mzige alisema kuwa elimu sahihi dhidi ya kupambana na maradhi hayo ya utapiamlo, yatatolewa kwenye kambi hiyo huku akisisitiza wazazi kujitokeza kwa wingi siku hiyo, kwani itakuwa ni ya kipekee na faida kwao na kwa watoto wao.
“Tujitokeze kupima afya zetu na pia watoto hasa wadogo. Hivyo kambi hii itakuwa msaada mkubwa kwani tutachunguza yale magonjwa mengi yanayowakabili watoto wengi hapa nchini.” Alisema Dk. Mzige.
Akitoa baadhi ya takwimu zinazowakabili watoto wengi hapa nchini, ni pamoja na :
Watoto 130, walio chini ya umri wa miaka 5 hufa kila siku hapa Nchini kwa ajili ya utapiamlo (Malnutrition-Lishe duni).
Upungufu wa wekundu wa damu asilimia 59 kwa watoto wenye miezi 6 hadi 59. Asilimia 33 ya watoto chini ya miaka 6 wana ukosefu wa vitamin A.

BANGO SANGHO, Dar es Salaam, Mwenyekiti wa umoja wa jamii ya watu kutoka India Bengali waliopo hapa Tanzania, BANGO SANGHO, Amit Nandy alisema kuwa kwa kushirikiana na Kliniki ya kimataifa ya afya ya uzazi kwa baba, mama, mtoto na vijana (AMM), ya Jijini Dar es Salaam ambapo wameandaa kambi hiyo ya kupima afya bila malipo kwa watoto wenye umri chini ya miaka 5 ni faraja kwa jamii hiyo kwani watoto wengi hapa Nchini wamesahulika katika kupimwa afya zao.
Amit Nandy aliwataka wananchi wa Kigamboni na maeneo mbalimbali kuwapeleka watoto wao katika shule ya Msingi, Kibugumu kwa ajili ya kupimwa afya zao hizo ikiwemo magonjwa yanayowakabili watoto wengi.
“wazazi wote tunawaomba kujitokeza kwa wingi, Machi 8, katika shule ya Msingi Kibugumu mukiwa na watoto wenu pamoja na makadi ya kliniki ilikuweza kupata huduma ya matibabu bure.
Madaktari bingwa na matabibu watapima magonjwa mbalimbali ikiwemo Afya ya kinywa, Uzito, Ukaguzi na ushauri wa lishe. Pia watakaobainika kuwa na matatizo maalum ya kiafya watapewa rufaa” alieleza Amit Nandy.
Ambapo alibainisha kuwa, huduma hizo za matibabu zinatarajiwa kutolewa kuanzia asubuhi ya saa tatu hadi saa saba mchana. (Saa 3:30 asubuhi-Saa 7-30 mchana).

0 comments: