Mahakama
nchini Pakistan imesesema adhabu ya kifo iliyotolewa kwa mwanamke
mkristo aliyeshtakiwa kwa kukufuru dini mwaka 2010 itatekelezwa.
Asia
Bibi alipatikana na hatia ya kutoa matamshi ya kukera na kuudhi kumhusu
Mtume Mohammad wakati akibishana na mwanamke mwingine muislamu.
Mahakama
kuu mjini Lahore, ilikataa rufaa yake dhidi ya hukumu aliyopewa na
mahakama ya chini. Mawakili wake wameahidi kuwasilisha kesi hiyo katika
mahakama ya juu zaidi nchini humo.
Hukumu iliyotolewa dhidi ya Bibi mwaka 2010 ilizua mjadala mkubwa kimataifa.
Wanasiasa
wawili wenye ushawishi waliuawa mwaka uliofuata baada ya kutoa wito wa
kubadilishwa kwa sheria dhidi ya kukufuru wakati kesi ya Bibi ilipokuwa
inaendelea.
Bibi alikanusha madai dhidi yake akisema kuwa mabishano yalitokea kati ya kikundi cha wanawake kuhusiana na nyungu ya maji.
Kukufuru
au kutoa matamshi ya kuudhi dhidi ya dini ya kiislamu ni swala tete
sana nchini Pakistan. Wakosoaji wanasema sheria dhidi ya kukufuru
hutumiwa vibaya na baadhi ya watu tofauti zinapoibuka na kwamba jamii
zilizotengwa ndizo hulengwa zaidi.
Tangu mwaka 1990, idadi kubwa ya wakristo wamefungwa jela kwa kukufuru au kukejeli dini ya kiislamu.
Wengi wao wamehukumiwa kifo na mahakama za chini huku nyingi ya hukumu zikifutiliwa mbali na mahakama za juu kwa kukosekana ushahidi wa kutosha.
CHANZO: BBC
CHANZO: BBC
0 comments:
Post a Comment