Wanachama
wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema katika kata ya Nkoarua Jimbo la Arumeru Mashariki na kata ya Sekei Arusha mjini kwa nyakati
tofauti wameandamana kwenye ofisi za chama chao kupinga majina ya
wagombea udiwani yaliyopitishwa wakidai kuwepo kwa ukiukwaji wa haki.
Wakizungumza kwa nyakati tofauti wanachama hao wanasema utaratibu
uliotumika kuwaondoa wagombea walioshinda kwenye kura za maoni
unakatisha tamaa na kuonyesha kuwa matakwa ya wengi hayazingatiwi hali
inayotishia uhai wa chama.
Kwa upande wa wagombea walioshinda na majina yao kukatwa Hagai
Kisila wa kata ya Sekei na Samwel Gipson wa kata ya Nkoarua wanasema
watafuata taratibu zote kuhakikisha kuwa haki inapatikana.
Viongozi wa Chadema wa wilaya ya Arumeru akiwemo Mwenyekiti
hawakuwa tayari kuzungumzia sakata hilo kwa kile kilichodaiwa kuwa wana
kikao kingine muhimu lakini kwa upande wa Chadema wilaya ya Arusha
mbunge wa jimbo hilo Godbless Lema amelazimika kuzungumza kwa niaba ya
viongozi ambao hawakuwepo.
0 comments:
Post a Comment