Wednesday, August 19, 2015

Wednesday, August 19, 2015
Kamati Kuu ya Halmashauri kuu ya Chama cha Mapinduzi imekamilisha kazi ya uteuzi wa wagombea ubunge katika majimbo mawili ya Singida Mashariki na Kiteto huku ikiteua kamati ya kampeni yenye watu 32 kwa ajili ya uchaguzi mkuu ujao.

Kamati hiyo itaongozwa na Katibu Mkuu wa chama hicho Bw Abdulrahiman Kinana. Kwenye majimbo hayo mawili CCM imewapitisha  Bw Jonathan Njau kwa jimbo la Singida Mashariki na Bw Emmanuel John kwa jimbo la Kiteto. Majimbo hayo yamechukuwa muda mrefu kujadiliwa na kutolewa maamuzi kwa lengo la kupata wagombea sahihi na wanaokubalika.
 
Akizungumzia suala la uvumi uliozushwa kwenye mitandao ya kijamii kuwa ameenguliwa kwenye nafasi hiyo ya ukatibu uenezi na kukabidhiwa Mh John Chiligati Bw Nape mbali na kulaani uzushi huo amesema wakati huu ndiyo umuhimu wa sheria ya mitandaoni inaonekana kwani ingekuwa imeanza kazi kero kama hizo zisingekuwepo.

0 comments: