Mwanamke anayeshukiwa ana Ebola akilia nje ya zahanati
Sierra Leone.
Rais wa Sierra Leone, Ernest Bai Koroma, ameteua tume
mpya ya kupambana na ugonjwa wa Ebola ambao umeuwa watu 1,200 nchini
humo.
Tume hiyo mpya itasimamiwa na waziri wa ulinzi, Meja Alfred Palo Conteh, na itaripoti moja-kwa-moja kwa Rais Koroma.
Taarifa
ya rais ilieleza kuwa alilazimika kufanya mabadiliko hayo kwa sababu ya
kazi kubwa ilioko ya kupambana na Ebola nchini Sierra Leone.
Umoja
wa Mataifa umeanza kusambaza chakula katika mji mkuu, Freetown, kwa
sababu watu wengi wanaogopa kutoka nje ya majumba yao wasije
wakaambukizwa ugonjwa huo.
Na Rais Obama ameonya watu wasiingiwe
na taharuki kubwa kuhusu ugonjwa wa ebola na alisema kuwa Marekani
haitazuia safari za ndege kutoka nchi za Afrika Magharibi
zilizoathirika na ugonjwa huo.
Rais Obama alisema hatua kama hiyo itafanya hali kuzidi kuwa mbaya.
Taarifa
hiyo imetoka wakati vyombo vya habari vya Marekani vinaarifu kuwa Bwana
Obama, faraghani, ameonesha hasira jinsi serikali yake
ilivvyoshughulikia msukosuko huo wa Ebola.
Ijumaa, mratibu wa
Umoja wa Mataifa kuhusu Ebola, David Nabarro, alitetea juhudi
zilizofanywa kimataifa kupambana na ugonjwa huo.
Bwana Nabbaro
alikuwa akijibu lawama za shirika la madaktari wasio na mipaka, MSF,
kuwa ahadi za kimataifa za matibabu na msaada, bado hazikupunguza mfumko
wa ugonjwa wa Ebola.
0 comments:
Post a Comment