Basi likiwa linasombwa na maji ya mafuriko
Mvua kubwa iliripotiwa kunyesha katika eneo la mji huo na viunga vyake mapema Alhamisi.
Katibu Mkuu wa shirika la Msalaba mMekundu Abbas Gulet anasema kuwa wamewaokoa watu 42 mpaka sasa.
Basi hilo liliondoka mjini Mandera kuelekea jijini Nairobi mapema siku ya jumatatu kabla ya kukwama katika matope.
Baadaye mvua kubwa ilinyesha na mafuriko kulisomba basi hilo.
Maafisa wa msalaba mwekundu wanasema kuwa wameanza kuwasaka watu waliotoweka katika mto mmoja ambao maji ya mafuriko hayo yanaelekea.
0 comments:
Post a Comment