Saturday, October 4, 2014

Saturday, October 04, 2014



MABINGWA wa Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, Azam FC wamepunguzwa kasi baada ya kulazimishwa sare ya bila kufungana na Prisons Uwanja wa Sokoine mjini Mbeya.Kwa sare hiyo, Azam FC inatimiza pointi saba baada ya kucheza mechi tatu na kushinda mbili- hivyo kuendelea kuongoza Ligi Kuu, ikifuatiwa na Mtibwa Sugar yenye pointi sita.Mtibwa Sugar watacheza kesho na Mgambo JKT ya Tanga Uwanja wa Manungu, Turiani, Morogoro mchezo ambao wakishinda watapaa kileleni.Katika mechi nyingine za ligi hiyo leo, Uwanja wa Jamhuri, Morogoro wenyeji Polisi wametoka sare ya 1-1 na Kagera Sugar. Polisi walitangulia kupata bao kupitia kwa Nicholas Kabipe dakika ya tano, kabla ya Rashid Mandawa kuisawazishia Kagera dakika ya 88.Uwanja wa Mabatini, Mlandizi mkoani Pwani, wenyeji Ruvu Shooting wametoka sare ya 0-0 na Mbeya City, wakati Uwanja wa Mkwakwani, Tanga Coastal Union wameshinda 2-1 dhidi ya Ndanda FC ya Mtwara.  Mabao ya Coastal yamefungwa na Joseph Mahundi dakika ya kwanza na Hussein Swedi dakika ya 26, wakati la Ndanda limefungwa na Nassor kapama dakika ya 57.Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, Simba imetoka 1-1 na Stand United ya Shinyanga. Bao la Simba limefungwa na Shaaban Kisiga la Stand limefungwa na Kheri Mohammed. Kikosi cha Azam FC kilikuwa; Aishi Manula, Shomary Kapombe, Gardiel Michael, Said Mourad, Aggrey Morris, Kipre Balou, Himid Mao, Salum Abubakar ‘Sure Boy’, Gaudence Mwaikimba, Didier Kavumbangu na Kipre Tchetche.Prisons; Mohamed Yussuf, Salum Kimenya, Laurian Mpalile, Nurdin Chona, Lugano Mwangama, Jumanne Elfadhil, Jeremiah Juma, Freddy Chudu, Ibrahim Hassan, Amir Omar na Julius Kwanga.


MATOKEO YA LIGI LEO: Simba SC 1-1 Stand Utd, Coastal 2-1 Ndanda FC, Polisi 1-1 Kagera Sugar, Prisons 0-0 Azam FC, Ruvu Shoot 0-0 Mbeya City.

.Kesho;Yanga SC Vs JKT Ruvu, Mtibwa Sugar Vs Mgambo.

0 comments: