Sunday, October 26, 2014

Sunday, October 26, 2014

 Kamishna wa Polisi Hamdan Omar Makame


JESHI la Polisi Tanzania limefanikiwa kukamata mabomu manne ya kivita yaliyofichwa katika eneo la mji wa Zanzibar na mtu ambaye jina lake limehifadhiwa kutokana na sababu za kiuchunguzi.
Akizungumza na waandishi wa habari jana makao makuu ya Polisi Zanzibar, Kamishna wa Polisi Hamdan Omar Makame alisema kuwa Polisi  wanaendelea na uchunguzi wa tukio hilo kwa kuwa uhalifu huo umewahi kujitokeza siku za nyuma.
Kamishna Makame alisema kuwa mtu amewekwa chini ya ulinzi na kuwaeleza polisi kuwa mabomu hayo yalikuwa matano lakini moja lililipuliwa katika eneo la Darajani mjini Unguja.
Makame kukamatwa kwa mtuhumiwa huyo kunatokana na ushirikiano baina ya polisi na raia wema ambao wamekuwa wakichukizwa na vitendo vya ulipuaji vinavyojitokeza katika nji huo.
Kamishna huyo hakuwa tayari kutaja jina la mtuhumiwa huyo wala eneo  waliokamata mabomu hayo kuhofia kuharibu uchunguzi na kutaka kuhakikisha vitendo vya kihalifu vinatoweka na watuhumiwa wanachukuliwa hatua za kisheria.
Februari 24, mwaka huu Watu wanne walijeruhiwa baada ya milipuko minne inayoaminika kuwa ni mabomu kutokea katika maeneo matatu tofauti Zanzibar.
Katika moja ya matukio hayo, watu wanne walijeruhiwa, mmoja akikatika mguu, katika eneo la Unguja Ukuu, Mkoa wa Kaskazini Unguja.

0 comments: