Wednesday, October 8, 2014

Wednesday, October 08, 2014
Zanzibar. Rais wa Zanzibar, Dk Ali Mohamed Shein amemtimua kazi Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar (AG), Othman Masoud Othman.
Hatua hiyo ya Dk Shein imekuja ikiwa ni wiki moja tangu mwanasheria huyo kukataa ibara 22 za Katiba inayopendekezwa wakati wa Bunge Maalumu la Katiba, mjini Dodoma.
Taarifa iliyotolewa jana na Katibu Mkuu Kiongozi Zanzibar, Dk Abdulhamid Yahya Mzee imesema Rais Shein amempandisha cheo aliyekuwa Naibu Mwanasheria Mkuu, Said Hassan Said kuwa AG.
“Amefanya mabadiliko hayo kwa mamlaka aliyopewa na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 kupitia Ibara ya 55(1), 53, 54(1) na 55(3)... Rais Shein ametumia Sheria ya Utumishi wa Umma ya mwaka 2011, Kifungu cha 12(3) na 27,” ilisema taarifa hiyo.
Othman ambaye hivi karibuni alijiondoa katika Kamati ya Uandishi ya lililokuwa Bunge Maalumu kwa kutoridhika na baadhi ya mambo, alieleza bungeni kutokubaliana na ibara ya pili, tisa, 86, 37, 70 hadi 75 na Sura ya 11 ambayo ina ibara ya 158 hadi 161, Sura ya 16 yenye ibara za 243 hadi 251 na Nyongeza ya Kwanza inayozungumzia mambo ya Muungano.
Hatua hiyo ilionekana kuwaudhi baadhi ya wajumbe ambao walimzomea na baada ya Bunge kuahirishwa, alitolewa kupitia mlango wa nyuma wa Ukumbi wa Bunge chini ya ulinzi mkali.
Baadaye Othman aliliambia gazeti hili kwamba licha ya kuwa yeye ni Mwanasheria Mkuu wa SMZ, alitumia utashi wake wa kidemokrasia kupiga kura kuzikataa ibara hizo, kutokana na kutoridhishwa na jinsi zilivyoandikwa.
“Katika suala la Katiba, Serikali ilishatamka kwenye Baraza la Wawakilishi na hata nje ya Baraza kwamba haina msimamo. Ndiyo maana uliona misimamo ilikuwa imeachwa kwenye vyama vya siasa, mimi siyo Mwanasheria Mkuu wa chama chochote.
“Kwa hiyo kama Serikali haikuwa na msimamo kwa maana ya upande… nilipiga kura kwa kuzingatia utashi wangu na maoni yangu.”
Ibara alizozikataa

Ibara ya 2. Hii inazungumzia eneo la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, likiwamo la Tanzania Bara na la Zanzibar pamoja na madaraka ya rais wa Jamhuri kugawa eneo lolote la nchi katika mikoa.

0 comments: