Thursday, October 2, 2014

Thursday, October 02, 2014

Waziri wa Uchukuzi, Dk Harison Mwakyembe

Serikali inatarajia kuanzisha usafiri wa treni kuanzia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa Julius Nyerere (JNIA) hadi katikati ya Jiji la Dar es Salaam, ili kupunguza adha kwa abiria wanaosafiri kwa ndege, ikiwa ni mkakati wa awali wa kuboresha na kuimarisha usafiri wa abiria kwa wakazi wa Jiji hilo.
Maandalizi ya usafiri huo wa kilomita 13 unatarajia kukamilika Disemba mwaka huu na kubeba abiria 800 hadi 1,000.
Hayo yalibainishwa jana na Katibu Mkuu wa Wizara ya Uchukuzi, Dk. Shaaban Mwinjaka, na kuwa  na kusema usafiri huo katika awamu nyingine utakuwa ni kuanzia mjini kuelekea Gongo la Mboto, Bagamoyo, Kibaha na Mkuranga.
Alisema kuwa wawekezaji ambao wamekwishafanya mazungumzo na serikali katika miradi mbalimbali katika maeneo ya bandari za Dar es Salaam pamoja na Mtwara ili kusaidia usafirishaji kutokana na kuwapo kwa uchimbaji wa gesi mkoani humo.
Maeneo mengine ni viwanja vya ndege vya kimataifa nchini, usafiri wa reli, soko la hisa pamoja na kuboresha kituo cha ukaguzi wa magari katika Taasisi ya Taifa ya Usafirishaji (NIT).
“Soko la hisa linakua kwa kasi nchini, wawekezaji hawa 12 wametoka nchini Marekani watakuwa katika miradi tofauti, na hii baada ya mazungumzo kati yetu na Marekani, kwamba tunahitaji wawekezaji katika maeneo tofauti na tulitoa kipaumbele katika kukabiliana na tatizo la ajali za barabarani tutaboresha kituo cha ukaguzi NIT kwa kununua vifaa, ” alisema Mwinjaka.
Alisema katika kuboresha ukaguzi wa magari kupitia NIT ili kukabiliana na ajali za barabarani, vinahitajika vifaa vya dola za kimarekani milioni 50 sawa na Sh. bilioni 85, pia vitafunguliwa vituo vya ukaguzi huo nchi nzima.
Pia alisema kuwa viwanja vya ndege vinavyopokea wageni wengi nchini kwa siku, vinahitaji kuwa na sehemu ya malazi na kupumzikia wageni na kusema ujenzi wa JNIA utakapokamilika utakuwa na huduma hiyo.
CHANZO:
NIPASHE     

0 comments: