Sunday, April 5, 2015

Sunday, April 05, 2015
    
    Meneja Mawasiliano wa TCRA, Innocent Mungy

WATUMIAJI wa mitandao ya kijamii nchini wametakiwa kujiandaa kutumia sheria mpya ya mawasiliano iliyopitishwa bungeni hivi karibuni.


Akizungumza na kituo cha redio cha Clouds, Dar es Salaam jana, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungy alisema kuwa kila mtu anatakiwa kutambua kuwa anawajibika katika matumizi ya mawasiliano.

Mungy alisema TCRA kwa kushirikiana na serikali, wataiweka sheria hiyo kwenye mitandao na kwamba kila mmoja anapaswa kuisoma na kuielewa.

Pia alisema wanajiandaa kutoa elimu kuhusu sheria hiyo na jinsi watumiaji wa mitandao ya kijamii wanavyopaswa kujihadhari ili wasije kuwajibika.

0 comments: